Friday, 18 November 2016
Mamlaka ya Bandari Bandari yapokea boti mbili za kuegesha meli
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepokea boti
mbili za kisasa za kuhudumia meli kutoka China zitakazotumika katika
Bandari za Dar es Salaam na Tanga.
Meneja Mawasiliano wa TPA, Janeth
Ruzangi alisema ujio wa boti hizo zilizopolewa jana utasaidia kuongeza
kasi ya utendaji kazi na ufanisi katika bandari hizo.
Alisema ujio wa
boti hizo ni sehemu ya mkakati wa TPA kuongeza vitendea kazi kwa upande
wa majini na nchi kavu ili kuongeza kasi ya upakuaji na upakiaji wa
mizigo kwa kiwango cha kimataifa na hivyo kuvutia wateja wengi.
Godbless Lema Akwama Tena Kupata Dhamana.......Arudishwa Gereza la Kisongo, Hatima Yake Kujulikana Wiki Ijayo
Hatma
ya dhamana ya Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema),
ilishindwa kujulikana jana baada ya mawakili wa Serikali kuweka
pingamizi, wakipinga Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha kusikiliza maombi ya
dhamana yaliyowasilishwa na mawakili wa mshtakiwa.
Kaimu
Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Jaji Sekela Moshi, alisema kutokana
na pingamizi hiyo, atasikiliza hoja za sheria zilizowasilishwa
mahakamani hapo kabla hajatoa uamuzi wowote juu ya dhamana ya mshtakiwa.
Aliwaelekeza mawakili wa pande zote mbili kuwasilisha hoja za sheria kabla mahakama haijaendelea na hatua yoyote.
Jaji Moshi alisema atatoa uamuzi kuhusu mvutano huo wa sheria, Novemba 22, mwaka huu
Wakuu 7 wa Mikoa Hatarini Kutumbuliwa kwa Kushindwa Kutekeleza Agizo la Rais Magufuli
Wakuu wa mikoa saba wako hatarini kutumbuliwa kutokana na kushindwa kutekeleza agizo la Rais John Magufuli kumaliza tatizo la madawati katika mikoa yao.
Akizungumza
jana alipokuwa akipokea madawati 3,500 yenye thamani ya milioni 300
kutoka benki ya NMB, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tamisemi, George
Simbachawene alisema mikoa ya wakuu hao saba inaoongoza kwa upungufu wa
madawati.
Aliwataja kuwa ni wa Geita, Mwanza, Kigoma, Mara, Rukwa, Simiyu na Dodoma.
Simbachawene alisema kutokana na kushindwa kutekeleza ahadi hiyo ametoa siku 43 na wasipotekeleza watakuwa wameshindwa kwenda na kasi ya Dk Magufuli.
Simbachawene alisema kutokana na kushindwa kutekeleza ahadi hiyo ametoa siku 43 na wasipotekeleza watakuwa wameshindwa kwenda na kasi ya Dk Magufuli.
Kamanda Sirro: Makonda ni Mwenyekiti wangu, Kama ana wasiwasi Atajua atachukua hatua gani dhidi yetu
Kamanda
wa Polisi mkoa wa Dar es salaam Simon Sirro, amesema kama Mkuu wa mkoa
wa Dar es Salaam Paul Makonda, ana wasiwasi na Jeshi la Polisi katika
operesheni ya kutokomeza matumizi ya Shisha, achukue hatua zaidi kwa
sababu yeye ni kiongozi wao na ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na
Usalama Mkoani Dar es salaam.
Thursday, 17 November 2016
Subscribe to:
Posts (Atom)






